Heri ni lie leo

Nimeona niwache kucheza na moto
Nitaangamia bure kwa joto
Kuinama mvunguni nikitamani chako
Nikujuchosha bure tako
Nimeona ni heri niinuke nigeuke nishike njia kutafuta change
Na basi kama siku hazigandi
Basi heri ni lie leo badala ya kesho kwani kesho
Langu laja

Chakuajabisha ni kwamba
Wataka kunivuta kwa kamba
Wajiona simba waniona mwiba
Nguvu zangu wazipima hujui nadunga!
Wataka niishi kama mmbwa!
Nikufuate huku na kule! Sitaweza! Nimechoka!
Ndio maana nasema heri nilie leo badala ya kesho
Kwani kesho langu laja

Hujatambua dunia ni duara
Aliyejuu mac Munga hushuka na aliye chini kapanda
Leo kwangu kesho kwako ushaskia hayo
Basi wacha niviringwe kwa shida
Machozi ya dondoke! Tsekha bhulamu bhwange
Sema mchana usiku kwa giza choma
Maliza risasi kwa bunduki! Fyatua! Fyatua!
Kesho langu laja!
Kesho nitang’aa utahitaji madigaga kuniangalia


© Namatsi Lukoye

Comments

Popular posts from this blog

Disrupt - Who am I

Love Is Not A Fight by Warren Barfield

Tick Tock Tick Tock